Wednesday 15 February 2017

Wachina hawamtaki fundi

Klabu ya Shandong Leung ya nchini China imekataa fununu zilizozagaa katika baadhi ya vyombo vya habari kwamba wao wapo kwenye harakati za kumsajili kiungo wa Chelsea na Hispania, Cesc Fabregas na wamesema kwa sasa hawahitaji mchezaji yeyote kutoka nje ya China.

Timu za China ziliwekea sheria ngumu kuhusu wachezaji kutoka nje ya China kwa vile zilikuwa na kasi ya kusajili wachezaji wengi kutoka haswa bara la ulaya ili kuweza kuongeza thamani ya soka lao.

No comments:

Post a Comment

Johnny MaLcom x

{picture#https://www.facebook.com/photo.php?fbid=1405295759685033&set=t.100007345536843&type=3&theater} The moment you come is the moment we let you go away {facebook#https://www.facebook.com/jeshilangu}
Powered by Blogger.