Friday 10 February 2017

Christian Atsu

Mmoja kati ya wachezaji ambao nategemea makubwa kutoka kwake. Anaitwa Christian Atsu Twasam akiwa na miaka 25 ambaye kiasili ni mtu wa Ghana. Sisi kama mashabiki wa Chelsea tunategemea makubwa kutoka kwake ingawa kwa sasa yupo kwa mkopo katika timu ya Newcastle united inayoshiriki ligi ya Championship ya Uingereza.

Amekuwa anafanya makubwa kwa timu zote ambazo amekuwa akicheza kama FC Porto, Everton na Newcastle kwa sasa.

Alisajiliwa na Chelsea mwaka 2013 akitokea FC Porto ambapo dau lake lilikuwa £ 3.5 milioni (paundi milioni 3.5) na akapelekwa kwa mkopo moja kwa moja nchini Uholanzi.

Style yake ya uchezaji haikosani sana na ya Victor Mosses ambaye naye alitua Chelsea akitokea Wigan Athletic na baada ya kutua Chelsea aliangaika sana kupata nafasi ya kucheza huku akipelekwa timu mbalimbali kwa mkopo kama Liverpool. Lakini kwa sasa amekuwa mchezaji tegemeo kwa Chelsea na hata timu yake ya taifa ya Nigeria.

Kwa maana hiyo basi Christian Atsu nae inabidi akaze buti ili kufikia mafanikio na baadae akaja kuwa bora.

No comments:

Post a Comment

Johnny MaLcom x

{picture#https://www.facebook.com/photo.php?fbid=1405295759685033&set=t.100007345536843&type=3&theater} The moment you come is the moment we let you go away {facebook#https://www.facebook.com/jeshilangu}
Powered by Blogger.