Antonio Conte kocha mkuu wa Chelsea amefanya mkutano na waandishi habari mchana wa leo kuelekea weekend ya muendelezo wa ligi kuu.
Kuhusu Eden Hazard kutakiwa
Conte; nadhani ni mchezaji mzuri na anaonekana anacheza vizuri muda wote hilo halina ubishi lakini sizani kama anauzwa.
*Akimaanisha Hazard hauzwi hii ni taarifa kwa Real Madrid na timu zinazomfukuzia.
Kuhusu mchezo dhidi ya Burnley
Conte: ni mchezo mzuri na Burnley wamekuwa na matokeo mazuri haswa wakiwa nyumbani, naamini wachezaji wangu watafanya kile kinachowapasa. Cha muhimu kuondoka na ushindi
*Nawaambia tu yule Tom Heaton pale golini ajiandae tu maana huu moto wa Chelsea sio wa mchezo
Kuhusu kuukaribia ubingwa
Conte: ni kweli tupo vizuri lakini hii isiwafanye wachezaji wangu wajisahau hapana bado tuna safari ndefu mbele yetu
*haters msituchukie yani hapa ni mwendo wa vipigo tu
Kuhusu Fabregas na Willian
Conte: ni wachezaji bora lakini sioni tatizo kwa wao kukaa benchi nadhani Pedro amekuwa bora sana
*yani hii Chelsea anatoka changarawe anaingia kokoto
Kuhusu safari yake alipoenda Juventus
Conte: ile haikuwa na maana yoyote zaidi ya kwenda kusafisha akili (relax) na kutoa uchovu. Nilienda kama matembezini tu
*ndo raha ya ushindi na kuwa bora unadhani leo eti Wenger asafiri bila mpango ataeleweka?
No comments:
Post a Comment