Mchezaji wa zamani wa Arsenal, Ian Wright ametoa neno kuhusu tetesi zinazomhusu Romelu Lukaku, akisema "kama mimi ndio ningekuwa Lukaku, basi kikubwa cha kufanya ningepanda na gari na kuchukua simu na kumpigia kocha (Koeman-kocha wa Everton) na kumwambia nipo njiani naelekea London(Chelsea)."
Romelu Lukaku ambaye ndie kinara wa mabao kwa sasa pale Uingereza akiwa na mabao 16 amekuwa akihusishwa na tetesi za kurudi Darajani ambapo ndipo alipotokea kabla na kujiunga na Everton anayochezea kwa sasa. Ambapo Chelsea ilimsajili kutokea klabu ya Ubelgiji iitwayo Anderlecht ambapo huko alikuwa mfungaji bora.
No comments:
Post a Comment