Tuesday, 1 August 2017

Mambo 4 unayopaswa kuyajua kwa kinda mpya Gilmour

Chelsea inaripotiwa kushinda vita juu ya kumsajili kinda anayetajwa kuwa na uwezo mkubwa, Billy Gilmour anayeichezea kwa sasa Rangers ya Scotland.

Chelsea inaripotiwa kutoa kiasi cha paundi 500,000 ili kumnasa kinda huyo mwenye miaka 15.

Na haya ndo mambo manne unayopaswa kuyajua juu ya mchezaji huyo.

1. Alibakiza kidogo kuweka rekodi ya kinda zaidi
Derek Ferguson ndiye anashikilia rekodi ya mchezaji kinda zaidi kucheza katika mechi ya kiushindani klabuni Rangers aliweka rekodi hiyo akiwa na miaka 16 na siku 24. Lakini kwa Billy Gilmour alibakiza kidgo kuivunja rekodi hiyo mara baada ya kuwa kati ya wachezaji wa akiba katika kikosi cha Rangers mapema mwaka huu ambapo alitimiza miaka 16 mwezi Juni tarehe 11. Kama angecheza kwenye mchezo huo aliokuwa mchezaji wa akiba basi angeweka rekodi hiyo ya kuwa kinda zaidi.

2. Rangers wameangaika kumzuia
Klabu inayomkuza mchezaji huyo ya nchini Scotland, Rangers imeshajalibu sana kumshawishi kinda huyo ili kuendelea kubaki. Lakini ilishawai kufika kwa wazazi wa mchezaji huyo ambapo kocha wa Rangers alifika na kuwashawishi wazazi waweze kumbakisha, ila wazazi waling'ang'ania kwamba mtoto wao ni lazima akacheze Chelsea.

3. Ana mafanikio makubwa kwenye soka
Akiwa timu ya taifa anayoichezea ya Scotland U-16 akiwa sambamba na kinda mwengine anayefukuziwa na Chelsea, Karamoko Dembele yule anayeichezea Celtic ilimenyana na Jamhuri ya Ireland U-16 katika mashindano ya vijana aliiwezesha timu yake kumaliza kama mshindi wa pili.

Lakini Billy Gilmour alisifika kwa uwezo wake wa hali ya juu katika unyumbulikaji wake na uwezo wa kutoa pasi.

4. Anaendana sana na mfumo wa Chelsea
Akademi ya Chelsea imekuwa na mafanikio makubwa katika kipindi hiki cha karibuni ikiwa imekuza vipaji vingi ambao mifano ya vipaji hivyo ni Charly Musonda, Nathaniel Chalobah na Ruben Loftus Cheek na kwa jinsi anavyocheza Billy Gilmour anaendana sana kimfumo na akademi ya Chelsea.

No comments:

Post a Comment

Johnny MaLcom x

{picture#https://www.facebook.com/photo.php?fbid=1405295759685033&set=t.100007345536843&type=3&theater} The moment you come is the moment we let you go away {facebook#https://www.facebook.com/jeshilangu}
Powered by Blogger.