Sasa ni Willy Caballero naye ameingia Chelsea mara baada ya kuhusishwa na kutua hapo kwa muda kidogo. Caballero amesajiliwa Chelsea akiwa kama mchezaji huru mara baada ya kumaliza mkataba na klabu yake ya zamani ya Manchester city.
Wakati Rudiger akitazamiwa kuja kuziba nafasi ya John Terry aliyeachwa na klabu, Willy Caballero anatazamiwa kuja kuchukua nafasi ya Asmir Begovic aliyejiunga na Afc Bournemouth.
Karibu Darajani shujaa wa kuokoa michomo ya penalty , Willy Caballero

No comments:
Post a Comment