Saturday, 29 July 2017

Conte hataki kufanya haraka kwa Hazard

Kocha wa Chelsea, Antonio Conte amesema hataki kufanya haraka kuwarudisha uwanjani wachezaji Eden Hazard na Tiemoue Bakayoko.

Conte alihojiwa kuhusu uwezekano wa wachezaji hao kuwai kurudi uwanjani kutokana na kuwa na majeraha lakini Antonio Conte alisema ni kweli tunawahitaji lakini hatuwezi kuwarudisha kwa haraka, cha muhimu ni wapone kabisa kisha ndo waungane tena na timu.

Eden Hazard aliumia akiwa anaitumikia timu ya taifa ya Ubelgiji wakati Bakayoko alisajiliwa akitokea Monaco kwa ada ya paundi milioni 40 akiwa na majeruhi.

No comments:

Post a Comment

Johnny MaLcom x

{picture#https://www.facebook.com/photo.php?fbid=1405295759685033&set=t.100007345536843&type=3&theater} The moment you come is the moment we let you go away {facebook#https://www.facebook.com/jeshilangu}
Powered by Blogger.