Goli hilo lilifanya mpaka mchezo huo kuisha kwa sare hiyo na kuzishuhudia timu hizo zikifika matuta.
Ndipo ule mfumo mpya wa matuta ukaanza kutumika, mfumo wa ABBA ambapo wa kwanza kupiga alikuwa mchezaji nahodha wa Chelsea, Gary Cahill aliyepiga vizuri na kufunga. Akafatiwa na mchezaji wa Arsenal, Oxlade Chamberlain aliyeifungia timu hiyo kwa tuta kabla ya Monreal kufunga tena. Baada ya hapo golikipa wa Chelsea Thibaut Courtois akapiga tuta ambalo lilipaa mbali na goli na kuifanya Arsenal kuongoza kwa matuta 3 kwa 1. Alvaro Morata naye akapiga akakosa, na hivyo kuifanya Arsenal kuwa na nafasi kubwa ambapo giroud alikuja kumaliza kazi kwa kupiga tuta tamu lililofanya Arsenal kushinda mchezo huo kwa matuta 4 kwa 1.

No comments:
Post a Comment