Tuesday, 7 March 2017

Chukua hii ya West Ham dhidi ya Chelsea, Je wajua?

Je unajua mechi baina ya West Ham dhidi ya Chelsea wamekuwa na matokeo ya kufanana msimu huu?

Timu hizo zimekutana mara tatu ndani ya msimu huu wa 2016-2017 na mchezo wa kwanza walicheza katika uwanja wa Stamford Bridge na Chelsea kutoka na ushindi wa 2-1.

Baada ya hapo zikakutana tena katika kombe la EFL na zikakutana katika uwanja wa London Stadium na wakaifunga Chelsea magoli 2-1.

Na jana ya tarehe 06-March wamekutana tena na Chelsea imeshinda 2-1.

Yaani katika michezo mitatu waliyokutana imeisha kwa idadi sawa ya magoli. Katika michezo hiyo Chelsea imeshinda michezo 2 na kufungwa na 1.

Chelsea imefunga magoli 5 katika michezo hiyo 3 na kufungwa magoli 3.

No comments:

Post a Comment

Johnny MaLcom x

{picture#https://www.facebook.com/photo.php?fbid=1405295759685033&set=t.100007345536843&type=3&theater} The moment you come is the moment we let you go away {facebook#https://www.facebook.com/jeshilangu}
Powered by Blogger.